Monday, December 03, 2012

WAANDISHI WATAKIWA KUACHA MAJUNGU NA KUFANYA KAZI KWA MASLAHI YA TAIFA.

MKUFUNZI WA SEMINA MWALIMU ROSE HAJI AKITOA DARASA KWA WAANDISHI WA HABARI MJINI KAHAMA.
KAHAMA
Uhusianao mbaya miongoni mwa waandishi wa habari ndiyo chanzo kikubwa cha kuporomoka kwa maadili ya taaluma ya hiyo nchini.
Hayo yamebainishwa leo na Mwandishi mkongwe nchini ambaye pia ni mkufunzi wa semina ya siku tano ya waandishi wa habari inayoendelea mjini kahama mama rose Haji Mwalimu kupitia shirika la UNESCO.
Haji amesema kuwa waandishi wa habari wengi nchini wamekuwa na chuki miongoni mwao hali inayopelekea kuchafuana na kujengeana uhasama katika vyanzo vya habari.
Ameongeza kuwa waandishi wa habari wanatakiwa kuweka ushindani katika kutafuta habari na kulikomboa taifa katika matatizo mbalimbali na si kijijengeana chuki hali, itakayopelekea kukosa uamnifu na kudhalaulika katika jamii.
Kwa upande wao waandishi wa habari wanaohudhuria mafunzo hayo wamekiri kuwepo kwa tabia hiyo kwa baadhi ya waandishi na kudai kuwa, sababu kubwa inayopelekea hayo ni baadhi ya watu kuingia katika fani ya uandishi pasipokuwa na taaluma.
Mafunzo hayo ya siku tano yanayojumuisha washiriki ishirini kutoka Redio za KAHAMA, FADECO ya KAREGWE,SENGEREMA ya MWANZA na ORKONEREI ya SIMANJIRO ni mwendelezo wa mafunzo ya uhariri na mipango ya vipindi chini ya mradi wa miaka mitatu unaoendeshwa  na shirika la UNESCO.

WAANDISHI WAKIENDELEA NA MAFUNZO

WAANDISHI KUTOKA VITUO VYA FADECO RADIO NA SENGEREMA WAKIENDELEA NA MAFUNZO.
WAANDISHI WA HABARI KUTOKA RADIO MBALIMBALI WAKIWA KWENYE CHUMBA CHA SEMINA.

KUTOKA KUSHOTO NI SEBASTIANE FURAHA WA RADIO KAHAMA,KATIKATI NI FEBRONIA BILIKWIJA WA RADIO SENGEREMA NA ENDRUE MFUNGO WA SENGEREMA FM.
KUTOKA KUSHOTO NI JOYCE ELIUS WA ORS FM,KIJUKUU CHA BIBI K WA RADIO KAHAMA FM,RACHEL LEMBURIS WA ORS FM NA AGNES UTOU
TOKA KUSHOTO KHADIJA KHASSAN WA KAHAMA FM,SEBASTIANE FURAHA KHM FM NAFEBRONIA WA SENGEREMA FM.

MKUFUNZI WA SEMINA MWL ROSE HAJI AKICHUKUA KUMBUKUMBU YA PICHA KABLA YA SEMINA KUANZA.

WASHIRIKI KUTOKA RADIO FADECO WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA.

No comments:

Post a Comment