Sunday, September 23, 2012

SAFARI YA WADAU KUTOKA KAHAMA HADI KARAGWE

Wadau watano wa ORS fm - Simanjiro tuliungana wadau wanne kutoka Kahama Fm kuelekea Karagwe - Kagera.

Tulipiga kambi kwa muda eneo linaloitwa BENAKO kwa ajili ya kupata chochote kabla ya kuendelea na safari

 William Bundala (Kijukuu cha bibi K) na Ramadhan Zuberi (Dj Rammy) kutoka Kahama fm, tuliungana nao kwa safari hiyo ya Karagwe.

 Julius Laizer, Agnes Utou na Kijukuu wakipata supu eneo la Benako

 Joyce Elias na Kijukuu wakiwaza kufika Karagwe, baada ya kuambiwa hakuna kuna shida ya usafiri kwa siku ya Jumapili kutoka Benako to Karagwe.


Wadau wakiwa bize, kubadilishana mawazo

 Tulikuwana naye Benako, alitustorisha hadi raha

Kijukuu akiangalia uchomaji wa ndizi na maganda yake - Tembea ujionee na kujifunza zaidi.

Safarini, mwendo wa zaidi ya saa 4 kufika Karagwe

 Geti la kwanza
 Unaweza usiamini, lakini ndivyo hali ilivyo kwa walinda usalama wa hii njia

 Mambo yetu yaleee ya dawa za kiasili

 Hapa ni kwenye geti la pili, nyumba kama hizo zipo saaaana hata mitaa fulani hivi kwa wale wenzetu

 Aaaah wewe usinipige picha bwana, ndivyo alivyokuwa akisema bwana Sadiq, safari tuliiona fupi sababu ya huyu jamaa, anaongea hakaukiwi maneno, much respect kwako bwana Sadiq kwa kampani yako.
Ulishawahi sikia pori ambalo Kamanda Tossi alikuwa anapambana na majangili, watekaji magari waliokuwa wanawaimbisha abiria Mtaji wa Maskini ni nguvu zake mwenyewe, ndio njia hiyo, asikwambie mtu hili pori hadi ulimalize na kufika salama Karagwe ni jambo la kumshukuru mungu, hapa tulisindikizwa na escort ya askari kwa kila geti wakipokezana hadi mwisho wa safari.

 Hatimaye tukaanza kuona unafuu wa kufika


 Kutoka kushoto ni Jackson Massawe (ORS fm) Sebastian Furaha a.k.a Seba, Khadija Hassan  - culture lady (Kahama fm) Julius Laizer, Khadija Abdallah, Agnes Utou (ORS fm) mwenye kofia ni Ramadhan Zuberi a.k.a Dj Rammy na aliyechuchumaa ni William Bundala - Kijukuu cha Bibi K (Kahama fm) tukipozi.

 Zao maarufu (Ndizi Bukoba, Matoke n.k) hapa ni njia ni tukielekea Kayanga.
 Panapendeza

 Tanzania yetu ni nzuri mnooooooo

 Aina ya upandaji Kahawa na Migomba

 Mambo ya msosi hayooooo. Ndizi zilizosongwa zimechanganywa na njegere, ndo msosi tulikaribishwa nao.

1 comment: